Wiki iliyopita, Baraka naye kwa upande wake alikana kuwepo kwa mahusiano ya kimapenzi na Nisha, akidai kuwa kusahau vitu vyake kwa mwigizaji huyo ikiwepo simu, ni vitu ambavyo hutokea na haimaanishi kuwa wana mahusiano.
Utafiti unaonesha kuwa, kuna hisia nzito na ukaribu mkubwa kati ya wasanii hawa wawili, kukiwa na dalili zote za mahusiano mazito ya kimapenzi, licha ya changamoto za hapa na pale, huku wasanii hawa wakikwepa kuweka wazi kinachoendelea kati yao na kuwapa mashabiki sintofahamu kwa makusudi.

No comments: